
Wakizungumza katika Ziara maalumu ya kuyakagua mabaraza hayo ya
Wilaya ya kaskazini A na B wamesema ili kujikwamua na hali gumu ya
maisha kwa vijana lazima wabuni miradi mbalimbali ikiwemo
kilimo,Uvuvi,Ufugaji,Ushoni ambayo itaweza kuwanyanyua na kuwapatia
ajira za uhakika.
Hata hivyo wamesema lengo la kushajihisha mabaraza hayo kubuni
miradi ni kwamba Serikali inamipango ya kuyainua mabaraza hayo kuanzia
ngazi ya Taifa, Wilaya hadi Shehia kwa kuyapatia mikopo itayoweza
kuendesha miradi yao waliyoibuni.
Nao Viongozi wa Mabaraza ya Vijana ya Wilaya wamesema licha ya
kuchukua hatua za kubuni miradi lakini bado wanarudisha nyuma na
baadhi ya vijana kutokuwa na utayari katika kujitolea kuendesha shughuli
za mabaraza na badala yake huyaona mabaraza hayo ni uwanja wa siasa.
Jumla ya Million mia 300 zimetengwa kwa ajili ya mabaraza ya vijana Zanzibar kwa Aajili ya kuendesha shughuli zao za maendeleo.
chanzo:Zanzibar24
Comments