Alisema takwimu za mwaka 2016 zinaonesha watoto 2,243 sawa na
asilimia sita hawakukamilisha chanjo ya kuzuia magonjwa ya dondakoo,
kifaduro, pepopunda, homa ya ini, homa ya uti wa mgongo na ugonjwa wa
kupooza. Masenza alisema takwimu hizo zinaonesha watoto 1,495 sawa na
asilimia nne hawakupata chanjo ya surua wakati watoto 5,979 sawa na
asilimia 16 hawakupata dozi ya pili ya kukamilisha hiyo.
“Kwa takwimu hizi inaonesha watoto wengi hawakupata au kukamilisha
chanjo zao kwa wakati na wapo kwenye hatari ya kupata maambukizi ya
magonjwa yanayozuilika kwa chanjo,” alisema.
Aliwataka wazazi na walezi
wenye watoto wa miaka chini ya mitano kuitumia wiki hiyo kuwapeleka
watoto wao katika vituo vya huduma ili wakapate huduma hiyo. Diwani
Bashiri Mtove, alisema, “Kata hii ambayo ukubwa wake ni kilometa za
mraba 162 ina zahanati moja tu na kwa mfano watu wa mtaa huu wa Msisina
ili wafike katika zahanati hiyo wanahitaji kutembea zaidi ya kilometa
12.”
Masenza aliahidi kuchangia Sh milioni moja kwa masharti kwamba,
lazima zahanati hiyo iwe na chumba maalumu kwa ajili ya huduma ya mama
na mtoto. Mratibu wa Huduma za Chanjo Mkoa wa Iringa, Naftal Mwalongo
alisema chanjo hizo zinatolewa ikiwa ni utekelezaji wa malengo endelevu
ya dunia yanayohusu afya ili kupunguza vifo vya watoto wa miaka mitano
ifikapo mwaka 2020.
chanzo:Habarileo.
Comments