Rais Kenyatta amewaambia waandishi wa habari kwamba, hatovumilia kitendo chochote cha kuchochea machafuko na kwamba sheria itamuadhibu vikali mtu yeyote atakayochochea machafuko na kujaribu kuvuruga uchaguzi huo.
Uchaguzi Mkuu unatarajiwa kufanyika tarehe 8 Agosti mwaka huu nchini Kenya. Ikumbukwe kuwa nchi hiyo ilishuhudia machafuko mabaya ya umwagaji wa damu baada ya uchaguzi mkuu wa tarehe 27 Disemba 2007. Mamia ya watu waliuawa na wengine wengine kupoteza makazi yao katika machafuko hayo.
Hivi sasa pia hali ya uchaguzi nchini Kenya ni ya wasiwasi kiasi kwamba machafuko yamekuwa yakiripotiwa katika chaguzi za michujo ya wagombea za vyama vya kisiasa nchini humo.
chanzo:parstoday.
Comments