Kaimu Jaji Mkuu aonya maamuzi kutafsiriwa nje ya mahakama.

Kaimu Jaji Mkuu Profesa Ibrahimu Juma.KAIMU Jaji Mkuu Profesa Ibrahimu Juma amesema kuwa wale wote wanaotoa tafsiri ya hukumu ama maamuzi yoyote ya kimahakama katika viwanja vya mahakama hapa nchini wanafanya makosa kwani wanaingilia uhuru wa muhimili huo.

Jaji Juma alisema hayo jijini Arusha alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika mafunzo ya siku tano yaliyohusisha Majaji wa Mahakama ya Rufaa, Majaji Wafawidhi na Majaji wa Mahakama Kuu namna ya kuboresha utendaji kazi wa mahakama.


Alisema mwenye mamlaka ya kutafsiri hukumu ama maamuzi ya mahakama ni Msajili wa Mahakama Kuu wa Kanda husika au mahakama na sio mtu mwingine yeyote.

Kaimu Jaji Mkuu alisema kuwa kinachofanyika sasa kwa wanasheria wa serikali na binafsi na wanasiasa kuzungumza na waandishi katika viwanja vya mahakama na kutafsiri kilichoamriwa na mahakama ni kuingilia uhuru wa mahakama na hakipaswi kufanyika tena.
chanzo:Habarileo.

Comments