
Mkuu wa Wilaya hiyo, Juma Homera amesema kutokana na wilaya hiyo
kuendelea kufanya vibaya kitaaluma na kuwa miongoni mwa wilaya
zilizofanya vibaya katika mitihani mbalimbali ya mkoa na taifa kutokana
na shuhuli hizo kufanyika zaidi wakati wa masomo jambo ambalo
linawakosesha masomo wanafunzi hao.
Akizungumza kwa njia ya simu, Homera alisema ni muda mrefu Wilaya ya
Tunduru iko nyuma kielimu ikilinganishwa na wilaya nyingine za Mkoa wa
Ruvuma huku chanzo kikitajwa ni mwamko mdogo wa elimu kwa wazazi, walezi
na jamii mzima ya watu wa wilaya hiyo.
Alisema kwa sasa timu ya viongozi ya Awamu ya Tano ikiongozwa na yeye
mwenyewe pamoja na wataalamu wengine wa halmashauri imeweka mikakati
kabambe kama vile kuhakikisha shule zote za msingi na sekondari zinatoa
chakula cha mchana kwa wanafunzi baada ya kubaini kwamba chanzo cha
kufanya vibaya na utoro kwa baadhi ya watoto ni kutopata chakula cha
mchana.
Alisema hakuna sababu ya msingi kwa Wilaya ya Tunduru kuendelea
kufanya vibaya kitaaluma kwa kwani ni kati ya wilaya zenye fursa nyingi
ambazo kama zikitumika vizuri zitasaidia kuharakisha kukua kwa uchumi
kuanzia ngazi ya familia, wilaya na mkoa..
Aidha, alisema kukamilika kwa
mtandao wa uhakika wa barabara ya lami kutoka Tunduru hadi makao makuu
ya mkoa mjini Songea na barabara kutoka Tunduru hadi Dar es Salaam
kupitia mikoa jirani ya Lindi na Mtwara ni fursa mojawapo ambayo inaweza
kuharakisha maendeleo.
chanzo: zanzibar24.
Comments