Chonjo alitoa agizo hilo juzi alipotembelea maeneo yaliyoathirika na
mafuriko ya mvua ambayo yalisababisha kaya 17 kwenye vijiji vya kata
hiyo kukosa makazi baada ya nyumba kubomolewa.
Mafuriko hayo ya mvua zilizotokea mwanzoni mwa Aprili mwaka huu
yamesababisha pia akiba ya chakula kilichokuwa kimehifadhiwa katika
nyumba hizo kuharibiwa na maji ikiwa na kuharibu ekari zaidi ya 20 za
mazao mbalimbali.
Mkuu huyo wa wilaya alisema licha ya kutokea kwa mafuriko hayo na
kuathiri baadhi ya kaya za wananchi katika kata hiyo, hali hiyo
imechangiwa pia na uharibifu wa mazingira kando kando ya mto na meneo
mengine ya milimani.
Kutokana na hali hiyo, alimwagiza Ofisa Mtendaji wa Kata hiyo
kusimamia sheria za mazingira kuhakikisha miti inapandwa eneo la mita 60
la mto na kabla ya kupanda miti hiyo alimtaka apate kwanza ushauri wa
aina ya miti inayofaa na rafiki wa mazingira.
“Eneo hilo la mita sitini kutoka kwenye mto kila upande ipandwe miti
na mpate kwanza ushauri wa wataalamu wa misitu wakiwemo wa Chuo Kikuu
cha Sokoine cha Kilimo (SUA) ili kuona ni aina gani ya miti inayofaa
kupandwa itakayokuwa ni rafiki wa mazingira,” alisema Chonjo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya
Morogoro, Sudi Mpili alisema athari za mafuriko hayo zimechangiwa na
uharibifu wa mazingira hasa maeneo ya mito na ukataji wa miti misitu ya
asili.
chanzo:Habarileo.
Comments