Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Agness amenyang’anywa simu
yake na kupigwa panga la kichwa wakati akiwa amejipumzisha nje ya nyumba
anayoishi maeneo ya Sogea Zanzibar.
Tukio hilo la kusikitisha limetokea juzi majira ya saa 5 usiku wakati
dada huyo alipokuwa amelala nje ya nyumba aliyopanga huku akiwa
ameshika simu yake mkononi ndipo alipotokea mtu asiyejulikana na kumpora
simu hiyo kisha kumpiga panga la kichwa na kumsababishia maumivu
makali.
Baada ya dada huyo kupiga kelele za kuomba msaada, majirani walitoka
na kumkuta ameshika maeneo ya kichwa huku damu zikiwa zinamtoka kwa
wingi na ndipo wakaamua kupeleka kituo cha polisi na baadae kumfisha
katika hospitali ya Mnazi mmoja kwa ajilia ya matibabu na hadi sasa hali
yake inaendelea vizuri .

chanzo:zanzibar24.
Comments