
Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Afya Harusi Said Suleiman wakati
alipokuwa akizindua wiki ya Chanjo ya Afrika huko Kituo cha Afya Kinuni
Mtofaani Wilaya ya Magharibi “A” Unguja.
Amesema chanjo hizo mpya ni pamoja na chanjo ya Nimonia na kuharisha
kwa watoto umri wa mwezi mmoja na nusu ambazo zinatolewa bure katika
vituo vyote vya Afya mjini na vijijini ili kuweza kuwakinga na maradhi
yanayojitikeza kila siku.
Alisema lengo la wiki ya chanjo Afrika ni kuongeza msisitizo juu ya
umuhimu wa chanjo katika kuokoa maisha ya watoto na kupata chanjo zao
kwa wakati uliopangwa.
Alisema kuwa Wizara ya Afya kupitia kitengo chake Chanjo imeweka
mazingira mazuri kuhakikisha huduma za chanjo kwa watoto zinapatikana
kwa urahisi na uweledi mkubwa katika vituo vyote.
Alieleza chanjo hizo zinazotolewa katika zoezi hilo zinajumisha aina
zote za chanjo za kawaida zinazotolewa kila siku katika vituo vya
ikiwemo Polio, kifua kikuu, Pepopunda, Dondakoo, Kifaduro, Homa ya Ini,
Homa ya Uti wa mgongo, Surua Rubella, Nimonia na Kuharisha.
“Wiki hii ina umuhimu mkubwa katika mustakbali wa maisha ya watoto
wetu hapa Zanzibar, sote kwa ujumla tuna jukumu la kuwalinda watoto wetu
dhidi ya maradhi mbalimbali kwa kuhakikisha wanapata chanjo zote
zinazostahiki tena kwa wakati uliopangwa,” alisisitiza Bi Harusi.
Naibu huyo alisistiza watoto wote walio chini ya umri wa miaka miwili
ambao hawakuweza kupata chanjo wapelekwe katika vituo vya afya kwa
ajili ya kupata chanjo hizo ambayo ni haki ya msingi kwa kila mtoto
kwani kukosa haki hiyo ni kumuhatarishia afya yake pamoja na maambukizi
ya maradhi .
“Takwimu za chanjo za mwaka 2016 zinaonesha kuwa bado kuna wilaya na
baadhi ya vituo vya afya havikufikia kiwango cha chanjo kilichotakiwa
hivyo nitoe wito kwa wilaya hizo na pamoja na vituo vyote vya afya
vitumie nafasi hii ya wiki ya chanjo Afrika kuhamasisha jamii na familia
kuhusu umuhimu wa kupata chanjo hizo,”alieleza Naibu huyo wa Afya
Hata hivyo Naibu Harusi alifahamisha kuwa Serikali inategemea kuanza
kutoa huduma ya chanjo ya kujikinga na saratani ya shingo ya mlango wa
kizazi kwa kina mama wenye uwezo wa kuzaa ifikapo mwaka 2018 hivyo ni
jukumu la kina mwananchi kuelimishana juu ya umuhimu wa chanjo.
Hata hivyo amliwataka viongozi na watendaji wa ngazi zote kutoa
ushirikiano katika kuhakikisha kuwa wananchi wanahamasika katika kushiki
chanjo hizo ili kufikia lengo lililokusudiwa la kutokomeza maradhi kwa
watoto.
Akitoa maelezo mafupi kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara ya Kinga bi
Atie Juma Shaame alisema serikali inachukua juhudi kubwa katika kupiga
vita na kuondoa maradhi kwa kutoa chanjo dhidi ya watoto hivyo
wananchi wasipuuze kuwapeleka katika vituo vya afya ili kuweza kupata
Taifa bora lenye afya njema.
Alisema chanjo ni kitu muhimu kwa maisha ya binadamu katika kujikinga
na maradhi mbalimbali ambayo itamwezesha kuishi katika afya nzuri na
kuepukana na maambuzi yanayoweza kuepukika.
Nae Mwakilishi kutoka Shirika la Kuhudumia watoto Duniani UNICEF
Shemsa Nassor Mselem amesema shirika lake litaendelea kutoa ushrikiano
na serikali ili kuhakikisha kuwa kila mtoto anapata chanjo ambayo ni
haki yake ya msingi na hasa wale wanaoishi katika mazingira hatarishi
wasikose kupata haki yao hiyo.
IMETOLEWA NA MAELEZO ZNZ.
chanzo: zanzibar24.
Comments