
Akizungumza na Zanzibar24 Afisa Mazingira wa baraza hilo Jaku
Abdalla Jaku amesema katika kipindi cha mvua maradhi ya miripuko
hujichomoza kutokana na mazingira kuwa machafu hivyo ili kuepusha na
kunusuru afya za wananchi mfanyabiashara watakao
gundulika anakwenda
kinyume katika kudhibiti mazingira maeneo yao ya biashara yatafungiwa
bila ya kumuonea muhali.
Hata hivyo amesema baraza la manispaa limeanza kufanya ukaguzi nyumba
kwa nyumba ili kuwachukulia hatua za kisheria wananchi waliokuwa
hawana karo za kutunzia maji machafu kwani maji hayo huhatarisha afya
kwa jamii.
Aidha amesema wamekuwa wakitoa elimu kwa wananchi lakini baadhi
yao imeonekana wanaizarau elimu hiyo ametoa wito kwa jamii kuwa na
mashirikiano katika kudhibiti mazingira ili kunusuru majanga
yanayoweza kuepukikana pamoja na kuwacha kutupa taka katika mitaro ya
maji machafu.
Jumla ya wafanyabiashara 20 wanatarajiwa kufikishwa Mahakamani kutokana na kukiuka masharti ya afya waliyopewa.
chanzo:Zanzibar24
Comments