Hata hivyo alidai wamekuwa wakipoteza muda wa masomo kwa zaidi ya
siku 45 kwa mwaka wakiwa katika hali hiyo.
Mkurugenzi huyo aliyasema
hivi karibuni wakati wa uzinduzi wa mradi mpya ujulikanao kama ‘usichana
wangu kwanza’ unaolenga kuwaelimisha wazazi na watoto wa kike pamoja na
kutatua matatizo yanayowapata wanafunzi shuleni kwa kipindi cha hedhi.
Kifunda alisema kuwa mradi huo wenye lengo la kutoa elimu kwa
wanafunzi wa kike wa shule za msingi na sekondari ambapo wamekuwa
wakiingia kwenye kupevuka bila kuwa na elimu ya afya, hali ambayo
imekuwa ikiwapa hofu na woga na kuwa watoro shuleni.
“Kupitia mradi wa
usichana wangu tutahakikisha tunatoa elimu ya afya kwa wazazi na
wanafunzi na kuzipunguza changamoto ikiwa imebainika zaidi ya asilimia
80 ya wasichana nchini wanaingia kwenye hedhi bila kuwa na elimu ya afya
yoyote , matokeo yake wanajawa na hofu kubwa na woga, hali ambayo
inasababisha utoro mashuleni,” alisema.
Baadhi ya walimu akiwemo mwalimu kutoka shule ya sekondari Kishapu,
Stephen Cleophas alisema kuwa muda mrefu changamoto hiyo imekuwa
ikisababisha wanafunzi wa kike kufanya vibaya katika masomo huku
wakiiomba serikali kushirikiana na wadau kuielimisha jamii juu ya
changamoto hiyo kwani imekuwa ikishusha kiwango cha elimu kwa wanafunzi
wa kike.
Ofisa Elimu Mkoa wa Shinyanga, Mohamed Kahundi alikiri kuwepo
kwa utoro mkubwa kwa wanafunzi wa kike shuleni, hali aliyoielezea ni
ukosefu wa elimu ya afya ya uzazi kwa watoto wa hao.
Alisema bado kuna tatizo la upatikanaji wa vitambaa vya kujisitiri
wanafunzi wa kike shuleni kwani bajeti inayotolewa na serikali
hatoshelezi mahitaji. “Asilimia 10 ya fedha za huduma ya kwanza katika
shule, haitoshi kuhudumia wanafunzi wote kwani shule zina wanafunzi
wengi ikiwa tunaendelea kuangalia namna ya watoto hawa ili waweze
kuhudhuria masomo yao,” alisema.
chanzo:Habarileo.
Comments