Akatwa mkono wa kushoto kwa kutolipa deni la shilingi laki tatu.

Mkazi mmoja wa Kijiji cha Keisangora Mkoani Mara, Mwita Magige, amekatwa mkono wake wa kushoto kwa kushindwa kulipa deni la Sh laki 3 alizokuwa akidaiwa.

Tukio hilo lilitokea baada ya ng’ombe wake waliokuwa wakichungwa na mkewe kukamatwa na mdeni wake ili kumshinikiza amlipe deni hilo.


Magige alisema, Aprili 5 akiwa safarini alipigiwa simu kuwa mifugo yake imekamatwa na uongozi wa Kijiji na alitakiwa kwenda kuikomboa, baada ya hapo alisitisha safari na kurejea nyumbani, alikwenda kwa Mwenyekiti wa Kijiji, Nuru Magacha alimweleza kuwa mifugo yake ipo na anadaiwa sh 300,000.

Magige alisema muda mfupi baadaye palipigwa mayowe kuashiria hatari huku akiwa hajui kinachoendelea, wananchi walikusanyika na ndipo  kijana mmoja alimkata mkono wa kushoto kwa panga na kuucha ukining’inia.
chanzo: zanzibar24.

Comments