Waziri Ummy alia na RC na DC kwa kuwasumbua Madaktari.

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amepiga marufuku Wakuu wa Mikoa na Wilaya(RC na  DC) kuwadhalilisha kwa kuwasweka lupango na kuwasumbua madaktari katika mikoa na wilaya zao.
Amesema kwa sasa imekuwa kama fashion kwa RCs na DCs kukamata watumishi wa umma hasa madaktari na kuwaweka ndani, vitendo vinavyopelekea kushusha morali ya kazi.

Ameongeza kuwa ameshakubaliana na Waziri wa TAMISEMI kuhusu kuwaelekeza Wakuu wa Wilaya na Mikoa mipaka yao ya kazi ili wasiingilie kazi na taratibu nje ya majukumu yao.
Agizo hili limekuja siku chache baada ya Mkuu wa Mkoa wa Singida kumuweka ndani DMO wa Singida na kusababisha daktari huyo kuandika barua ya kujiuzulu na kuacha kazi.
chanzo:zanzibar24.

Comments