Waziri wa kazi,Uwezeshaji,Vijana,Wazee,Wanawake na Watoto Moudline
Cyrus Castico amesema serikali imedhamiria kuweka mikakati ya kuimarisha
hali ya ustawi wa wanawake pamoja na kutoa fursa mbalimbali za
kumuwezesha wanawake kiuchimi.
Akizungumza na Waandishi wa habari ikiwa ni shamrashamra za kuelekea
siku ya wanawake duniani ambayo inatarajia kuadhimishwa kesho Jumatano,
amesema wanawake wamepewa kipaumbele katika fursa mbalimbali za
maendeleo ili kuhakikisha wanainuka kiuchumi kwa lengo la kujikimu
kimaisha.
Hata hivyo amesema licha ya kujitokeza vitendo vingi vya
udhalilishaji kwa wanawake na watoto ambavyo vinawarudisha nyuma
wanawake kimaendeleo lakini serikali haitokaa kimnya katika kupambana
na hali hiyo ili kumkombea mwanamke katika maisha duni na kumfikisha
katika maendeleo imara.
Wakati huo huo Wanawake kutoka Wilaya mbalimbali Unguja walifanya
kongamano la kuadhimisha siku ya wanawake duniani akiwemo Mtumwa Ali na
Arafa Juma Faki wamesema ili ya kujiinua kiuchumi kwa kuchukua mikopo
mbalimbali ya kimaendeleo ila wanarudishwa nyuma na kushindwa kupata
soko la kuuzia bidhaa zao na kutojua elimu ya biashara.
Siku ya wanawake duniani imekuja baada ya wanaharakati wa viwanda
walivoandamana kupiga kuonewa waliokuwa wakifanyiwa na waajiri wao
mwaka 1859 ambapo baada ya kuasisiwa umoja wa kimataifa mwaka 1945
baraza la umoja wa kimataifa ilitanga kila ikifika tarehe 8 March kila
mwaka ni siku ya wanawake duniani na kwaupande wa zanzibar imeaza
kuadhimisha tokea mwaka 1991 na Ujumbe wa mwaka huu ukiwa ni “Imarisha fursa za ajira kwa kumuwezesha wanamke kiuchumi”.
chanzo:Zanzibar24
Comments