Wawakilishi watoa maazimio 9 ya kupambana na madawa ya kulevya.

wawakilishiWajumbe wa baraza la wawakilishi wametoa maazimio tisa  kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar  katika kupambana na madawa ya kulevya nchini ili kutokomeza biashara hiyo inayo athiri nguvu kazi ya taifa ambayo  inaipa hasara kubwa kwa serikali.
Wakichangia  hoja binafsi  iliyowasilishwa na  Mwakilishi wa Jimbo la Mpendae Mohammed Said Mohammed
wajumbe hao ni Zulfa Mmaka Omar,Nadir Abdul-latif,Hassan Khamis Hafidh na Hussen Mohammed Makungu wamesema endapo serikali itafanya kazi kwa kushirikiana na jamii pamoja na wajumbe hao maazimiyo hayo yataweza kufanikisha katika kuwatia mbaroni waingizaji,wasambazaji na watumiaji wa madawa ya kulevya.
Akisoma maazimio yaliyoungwa mkono na wajumbe wa baraza hilo Mohammed Said Mohammed Dimwa amesema Serikali ihakikishe  inasimamia  vyema sheria namba 9 ya 2009 ya  kuzuia  biashara haramu ya dawa za kulevya  bila ya kumuonea mtu muhali ili kulinusuru taifa.
Jumla ya kesi 569 zilizofunguliwa za madawa ya kulevya kwa mda wa miaka minne iliyopita  kutoka 2013 hadi 2016.
Chanzo:Zaznibar24

Comments