Mh, Mkuu wa Wilaya ameyasema hayo
wakati alipokuwa, akizindua zoezi la utoaji wa chanjo ya kichaa cha Mbwa huko
Shehia ya Konde, Wilaya ya Micheweni, Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Mkuu wa Wilaya amesema kuwa, kuna watu wanatabia
ya kudharau maagizo ya Serikali wakiyahusisha na siasa jambo ambalo ni
kinyume ya malengo yaliokusudiwa na kupelekea madhara makubwa kwa
jamii.
Akitoa maelezo mafupi juu ya umuhimu na malengo ya
njanjo za Kichaa cha mbwa.
Afisa Mipango wa Idara ya Maendeleo ya
Mifugo Pemba
Suleiman Hamadi Hija, amesema kuwa, lengo la kutoa
huduma hiyo ni kutokomeza ugonjwa wa Kichaa cha Mbwa ambao
unaathiri kwa kiasi kikubwa maisha ya Wanadamu na Wanyama kiujumla.
Afisa mipango huyo amesema kuwa, kumekuwa
kukiongezeka matukio ya watu na Wanyama kuumwa na mbwa siku hadi siku katika
Wilaya Micheweni kutokana na mwitiko mbaya wa jamii katika kipindi
cha uchanjaji wa
Mbwa mwaka uliopita.
Nae Mfugaji wa Mbwa, Kutoka Sehiya ya Konde, Sadam
Said Ali, alisema kuwa Serikali imewasaidia kwa hatua kubwa
kuwapatia huduma ya chanjo ya kichaa cha Mbwa, bila ya malipo, ili kusaidia
usalama wa afya zao.
Huduma ya utoaji wa chanjo ya Kichaa cha Mbwa
ambayo ilifanyika mwezi Septemba mwaka jana katika Wilaya zote nne kwa
Pemba, ni Wilaya ya Micheweni Pekee ambayo imekuwa ikiripotiwa matokeo
ya watu kuumwa na Mbwa kuanzia Januari hadi kufikia idadi ya watu
38, Machi 13 Mwaka huu, kutokana na kutoitikia wito kikamilifu kupata
huduma hiyo.
Comments