Wanawake wa jamii ya wafugaji wa Barbaig wamelalamikia vitendo vya udhalilishaji wanavyofanyiwa na Polisi.

Wameyasema hayo mbele ya viongozi wa serikali katika mkutano wa
kutafuta suluhu ya maiti zilizoachwa kuzikwa sababu ya tofauti ya polisi
na wabarbaig hao.
Katika mkutano huo, polisi wametuhumiwa kuwa wamekuwa wakiiba unga wa
mahindi kwenye mabanda ya wafugaji, kuiba maziwa, simu na vitu vyenye
thamani wanapovamia na kuchoma nyumba za wafugaji.
Aidha Wabarbaig hao wameomba kila kiongozi wa serikali anapoenda
kuwaondoa wafugaji awe anawatajia eneo mbadala na si kuwafanyia ukatili.
chanzo: zanzibar24.
Comments