Wananchi watakiwa kupunguza uharibifu wa mazingira

Wananchi wametakiwa kupunguza uharibifu wa mazingira ambao umesababisha kuongezeka kuwepo kwa athari zinazotokana na mabadiliko ya hali ya hewa na kupelekea kilimo na mazao kuathirika zaidi.

Akizungumza katika Mafunzo  ya asasi za kiraia juu ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi,
Mratibu wa Jumuiya ya ZACCA Soud Mohammed Juma amesema kutokana na utafiti uliofanywa imeonekena maeneo mengi ya  Zanzibar yameathiriwa na mabadiliko ya hali ya hewa   hasa katika maeneo  ya kilimo kwa kuvamiwa na maji ya bahari, maji ya visima kugeuka ya chumvi pamoja na kuongezeka kwa gesi joto.

Nao washiriki wa mafunzo hayo wamesema kutokana na hali hiyo basi ipo haja kwa serikali  kwa kushirikiana na asasi za kiraia kudhibiti  mabadiliko hayo kwa  kuchukua hatua za haraka kwani elimu tayari imeshatolewa lakini bado jamiii haijawa tayari kushirikiana na kuendelea kufanya vitendo vya uharibifu wa mazingira.

Kwaupande wake Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohammed Mahmoud amesema Serikali tayari imetilia mkazo kwa kuchukua hatua za haraka kudhibiti kwa njia ya kuhifadhi misitu pamoja na kuotesha vioto vya asili na elimu zinatolewa ili kupunguza  mabadiliko hayo.
chanzo:Zanzibar24

Comments