Duru za kiusalama za Somalia zimetangaza kuwa jeshi la nchi hiyo jana
Ijumaa lilitekeleza oparesheni karibu na mji wa bandari wa Kismayo
katika jimbo la Jubaland na kuwauwa wanamgambo sita wa kundi la al
Shabab.
Duru hizo zimesisitiza kuwa oparesheni hiyo ya jeshi ambayo imeanza
kwa lengo la kuharibu maficho ya kundi la al Shabab itaendelea katika
siku zijazo.
Kundi la kigaidi la al Shabab linaendelea kufanya mashambulizi dhidi
ya raia na askari usalama huko Somalia licha ya jeshi la nchi hiyo
kuendesha operesheni ya kuwaangamiza wanamgambo wa kundi hilo nchini
humo.
CHANZO: parstoday.
Comments