Mjumbe wa Bunge la Palestina Bi. Samira al Halayka ambaye ni mwanachama wa Hamas, alikamatwa Alhamisi akiwa nyumbani kwake katika mji wa al-Shoyoukh katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
Duru zinadokeza kuwa mbunge huyo alifungwa pingu kisha akafunikwa macho na kupelekwa kusikojulikana na wanajeshi hao wa Israel.
Taarifa zinasema wanajeshi wa Israel pia walipora kompyuta yake na simu yake ya mkononi katika oparesheni hiyo ya utekaji nyara.
Baada ya kutekwa nyara al Halayka, idadi ya wabunge wa Palestina wanaoshikiliwa katika korokoro za Israel imeongezeka na kufika 10.
chanzo:parstoday.
Comments