Wakulima waiomba Serikali kuwapatia elimu ya kuzalisha bidhaa zinazoendana na mahitaji

Wakulima wa kijiji cha kilindi kilichopo Wilaya ya Kaskazini  A wameiomba wizara ya kilimo kuendelea kuwapatia elimu ya kuzalisha bidhaa zinazoendana na Mahitaji ya nchi ili waweze kunufaika na kilimo wanacholima.

Wakizungumza na Zanzibar24 huko katika Shamba la kuzalisha mimea ya kilimo, Sheha wa shehia ya kilindi Ali Omar Mussa na mkulima Maryam Hamad
wamesema mbali na kupokea mafunzo ya kilimo kupitia Mradi wa kaya masikini TASAF lakini wanahitaji mafunzo zaidi ili waweze kuzalisha mazao yenye kiwango.

Aidha wamesema uwepo wa mradi wa TASAF umewawezesha kujikwamua kiuchumi na kuweza kutumia njia za asili katika kilimo bila ya kutegemea mvua pamoja na kuwa na ujuzi wa kutengeneza mbolea ambayo ni salama kwa watumiaji wa mazao yanayozalishwa.

Kwa upande wake Muwezeshaji wa Vikundi vya mbogamboga na matunda kutoka TASAF Fatma Mwinyiwesa Idarusi amewambia wanakijiji hao kuzidi kuitumia ipasavyo elimu wanazopewa katika kilimo ili kuweza kulinda afya zao pamoja na kujiendeleza kiuchumi .

Miongoni mwa kilimo wanacholima wanakijiji  hao ni Migomba na mboga mbaoga ikiwemo pilipili, spinach na Matango.
chanzo: Zanzibar24.

Comments