Pia imezitaka taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi
na Mawasiliano kutumia kituo hicho katika kutunza kumbukumbu zake ili
kuwa mfano kwa taasisi nyingine za umma.
Akizungumzia maazimio ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu
baada ya ziara ya siku moja ya kuitembelea Kampuni ya Simu Tanzania
(TTCL) pamoja na miradi ya Mkongo wa Taifa na Kituo Mahiri cha Kutunzia
Kumbukumbu, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Norman Sigala alisema
uhai wa TTCL upo mikononi mwa serikali.
Aidha, Kamati hiyo ya Bunge imezitaka taasisi zote za umma na binafsi
kulipa madeni inayodaiwa na TTCL kuiwezesha kampuni hiyo kujiendesha
kwa ufanisi.
Mjumbe wa Kamati hiyo, Rita Kabati alisema kukamilika kwa mchakato wa
kuondoka kwa Bharti Airtel ndani ya TTCL kunahitaji kwenda sambamba na
uwezeshaji wa mtaji kama ilivyofanyika kwa Kampuni ya Reli Tanzania
(TRL) na Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) ambazo sasa zinafanya vizuri.
Chanzo:Habarileo.
Comments