Vuai Ali Vuai: Sina nia ya kuhama CCM.

Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai, amesema licha ya kuvuliwa nyazifa yake hiyo lakini bado hana nia ya kukihama chama hicho kama baadhi ya watu wanavyodhania.

Amesema kuwa kuna baadhi ya watu wanaonekana kuwa na mitazamo tofauti kwake, akisema kuwa watu hao wameanza kuingia wasi wasi wa kuona kama hatua hiyo inaweza kumfanya kuvunjika moyo katika kuunga mkoni jitihada za chama hicho na kuamua kung’atuka ili kukwepa aibu kwa baadhi ya wanachama.


Amesema suala hilo halina nafasi kwa upande wake hata kidogo, akidai kuwa kuondolewa nafasi hiyo ni sehemu ya uimarishaji wa chama hicho.

Aidha ameongeza kuwa, mabadiliko hayo ameyapokea kwa mikono miwili na wala hana chuki na Mwenyekiti wa Chama hicho John Magufuli ambaye ni msimamizi wa shughuli zote.

Hata hivyo amesema kuwa pamoja na kuizoea nafasi hiyo lakini bado hajaathirika katika utendaji wake wa majukumu katika chama hicho na kuahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya kukisaidia chama chake.

Hata hivyo amesema ataendelea kutoa ushirikiano wake ndani ya chama hicho ili waweze kupiga hatua zaidi za kukiimarisha chama chao.

chanzo: zanzibar24.

Comments