Baadhi raia wameuelezea mji wa Bowen kwamba umeharibika na kuwa kama ukanda wa vita kutokana na kubomoka kwa majengo na mashamba ya ndizi.
Waziri mkuu wa Australia Malcolm Turnbull, amesema kuwa serikali imejiandaa vyema kukabiliana na madhara ya kimbunga hicho kilichoyakumba maeneo hayo.
Hata hivyo mamlaka nchini Austarilia zimeonya kuwa eneo la Pwani ya kaskazini mashariki nchini humo lililopo kilomita 1300 linatarajiwa kukumbwa na mafuriko ikiwa ni matokeo ya kimbunga hicho.
chanzo:Bbc.
Comments