
Mjumbe wa Kamati Kuu na Katibu Mkuu wa Chama cha Kikomunisti cha
China (CPC), Guo Jinglong
aliyasema hayo katika mazungumzo kati yake na
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed
Shein ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Zanzibar, huko Ikulu mjini Zanzibar.
Kiongozi huyo ambaye yuko ambaye yuko nchini, amempongeza Dk. Shein
kwa juhudi zake za kuoingoza Zanzibar na kuweza kupiga hatua kubwa za
maendeleo sambamba na kuimarisha amani na utulivu hapa nchini na
kusisitiza kuwa hatua hiyo ya kuziunga mkono sekta hizo za maendeleo
ikiwemo ujenzi huo wa jengo hilo jipya la abiria katyika uwanja wa ndege
wa Zanzibar kutaimarisha sekta ya utalii.
Alisema kuwa tokea Dk. Shein kuweko madarakani Zanzibar imeendelea
kupiga hatua kubwa za maendeleo na kuongeza kuwa kuchaguliwa kwake tena
na wananchi kwa kipindi cha pili madarakani kuendelea na wadhifa wake
huo kumezidi kuiletea maendeleo Zanzibar.
Kiongozi huyo alimueleza Dk. Shein kuwa Serikali ya Jamhuri ya Watu
wa China pamoja na chama chake cha CPC kimekuwa na uhusiano wa muda
mrefu na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Chama Cha
Mapinduzi (CCM).
Kiongozi huyo wa CPC alimueleza Dk. Shein kuwa hakuna sababu ya
kuvunjika kwa uhusiano huo uliopo na kueleza dhamira ya Serikali yake
kuendelea kutoa ushirikiano kwa Zanzibar pamoja na kuendelea kukiunga
mkono Chama Cha Mapinduzi.
Kuhusu sekta ya afya Kiongozi huyo alieleza kuwa China itaendelea na
utaratibu wake wa kuleta madaktari hapa Zanzibar kwa kila baada ya muda
uliopangwa ili kuimarisha utamaduni huo ambayo ulianzishwa tokea mwaka
1965.
Katibu Jinlong alisifu jitihada zinazoendelezwa na CCM ambazo zina
itikadi zinazofanana na CPC hatua inayoonesha wazi ukomavu wa CCM
kisiasa ambayo inawafanya wananchi walio wengi waendelee kukiamini chama
hicho kutokana na Sera zake imara za maendeleo kwa ajili ya kuimarisha
ustawi wa wananchi wa Tanzania bila ubaguzi.
Aidha, alieleza umuhimu wa viongozi wa vyama vya CCM na CPC
kutembeleana ili kubadilishana mawazo na kuimarisha uhusiano na umoja
wao wa kihistoria uliopo kati ya vyama hivyo.
Sambamba na hayo, Mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya CPC alitoa pongezi kwa
wananchi wa Zanzibar, Serikali na Chama Cha Mapinduzi kwa mapokezi
mazuri waliyoyapata wakiwa hapa nchini yeye na ujumbe wake.
Nae Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali
Mohamed Shein alitumia fursa hiyo kutoa pongezi kwa ujio wa kiongozi
huyo hapa nchini na kusisitiza kuwa hatua hiyo ni uhusiano mwema na
ushirikiano uliopo kati ya CCM na CPC pamoja na Serikali za China na
Tanzania.
Dk. Shein alisema kuwa azma ya China kuendelea kushirikiana na
Zanzibar katika kuimarisha miradi ya maendeleo ukiwemo mradi wa ujenzi
wa bandari ya Mpigaduri na uwanja wa ndege wa Abeid Amani Karume
kutaimarisha ukuaji wa uchumi sambamba na kuimarisha sekta ya utalii.
Alieleza kuwa asilimai 80 ya fedha za kigeni zinatokana na mchango
mkubwa wa sekta ya utalii ambayo pia, huchagia asilimai 27 ya pato la
Taifa.
Aidha, Dk. Shein alisisitiza kuwa Zanzibar imekuwa na uhusiano na
China tokea wa kihistoria kati yake na China hatua ambayo imewapelekea
wananchi wa China kuweza kuishi Zanzibar na kuwa Watanzania hivi sasa.
Aliongeza kuwa Serikali ya China imeweza kuiunga mkono Zanzibar
katika sektra mbali mbali za maendeleo ikiwemo sekta ya kilimo ambapo
mara tu baada ya Mapinduzi matukufu ya Janurai 12, 1964 ambayo China ni
miongoni mwa nchi za mwanzo kuyatambua ambapo pia, Serikali hiyo
ilianzisha kilimo cha umwagiliaji maji hapa nchini.
Aidha, China ilijenga viwanda mbali mbali kikiwemo kiwanda cha
sigara, kiwanda cha viatu pamoja na viwanda vidogo vidogo sambamba na
kuleta wataalamu wa fani mbali mbali hapa Zanzibar.
Kwa upande wa sekta ya afya, Dk. Shein alisema kuwa serikali ya China
imeweza kuunga mkono sekta ya afya kwa kuleta wataalamu wa sekta hiyo
tokea mwaka 1965, na ujenzi mpya wa hospitali ya Abdalla Mzee pamoja na
vifaa kwa hospitali hiyo na hospitali ya MnaziMmoja.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
chanzo:zanzibar24.
Comments