Save the Children: Waandishi wanapaswa kufuata maadili kuepuka kudhalilisha watoto.

Waandishi na vyombo vya habari  wametakiwa  kuzingatia zaidi maadili na haki za mtoto pale wanapoandika au kutangaza habari zinazowahusu  watoto ili kuepusha  udhalilishaji  dhidi yao.
Akitoa Mafunzo kwa waandishi wa habari Mwakilishi kutoka shirika la kimataifa linalosaidia watoto  Save the Children
Ellen Otaru amesema hivi sasa waandishi wengi nchini pamoja na vyombo vya habari vimekuwa vikiandika habari mbalimbali zinazowahusu watoto ambapo hufanya udhalilishaji bila ya kujijua hivyo ipo haja ya kuzingatia maadili na kanuni za uwandishi hasa katika kutoa taarifa za udhalilishaji ili kuepuka nayeye kumdhalilisha mtoto.
Hata hivyo amesema ili kuepuka makosa hayo waandishi wanapaswa kuandika taarifa zisizo na ukinzani na kuepuka kutoa picha ambazo zinaharibu maadili na haki ya mtoto, kumpa uhuru mtoto wa kuongea  pindi anapopata tatizo bila ya kutumia nguvu au hongo kwa watoto ili kutoa taarifa.
Naye Mwakilishi kutoka chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania kwa upande wa Zanzibar Grace Ngonyani amesema  sheria ya elimu  ya namba 6 ya  mwaka 1982 bado inachangamoto kubwa kwa mtoto kwani humnyima fursa pale anapopata ujauzito au kuolewa kuweza kurudi tena skuli hivyo vyombo vya sheria lazima iifanyie marekebisho ili kuweza kumpa haki yake mtoto ya kupata elimu.
chanzo: Zanzibar24

Comments