Polisi wadaiwa kuua wafugaji Bagamoyo.

Vijana wawili wa jamii ya wafugaji wamefariki dunia kwa kupigwa risasi na polisi waliokamata kwa kukutwa na mifugo inayozaniwa kuwa ni ya wizi.


Katika tukio hilo, askari mmoja amejeruhiwa kwa kuchomwa mkuki.



Tukio hilo limetokea eneo la Relini katika Kijiji cha Kidomole, Kata ya Fukayosi.



Akizungumza na Gazeti hili, Diwani wa Fukayosi, Ally Ally aliwataja vijana hao ambao ni ndugu, kuwa ni Sainga Gheambalelega (21) na Rumay Gheambalelega (23).


Diwani huyo amesema chanzo cha tukio hilo ni baada ya vijana hao kuwagomea askari kuswaga ng’ombe hao wanaodaiwa kuibiwa kwenye zizi la mfugaji mwingine jina linahifadhiwa kwa uslama.



Diwani huyo amesema awali, polisi walipokea taarifa kutoka kwa mtu huyo aliyedai kaibiwa mifugo yake na ameiona katika moja ya maboma ya wafugaji wenzake eneo la Relini.



“Ndipo polisi wakaondoka kwenda kuiswaga wailete kwenye kituo chao wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani. Wakiwa njiani ndipo kundi la  wafugaji liliwavamia na kuanzisha vurugu,” amesema diwani huyo.



Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Boniventura Mushongi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na ameahidi kulitolea ufafanuzi kesho.


Chanzo:Mwananchi.

Comments