Nape: Sijakamatwa na Polisi....Nipo Protea.

Baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli leo kutengua uteuzi wa Waziri  wa Habari, Sanaa, Utamaduni na michezo, Nape Nnauye....Mbunge huyo yupo hotel ya Protea tayari kwa kuongea na waandishi habari kuhusu kutumbuliwa.

Akiwa njian kuelekea Protea, silisambaa habari kwamba amekatwa. Taarifa hizo amezikanusha kupitia mtandao wa twitter na kudai yuko salama.

Wanasambaza nimekamatwa! Niko njiani nakwenda Protea, niko salama nimetoka Arusha na ndege mchana huu! Nashauri waache UONGO, WATULIE!

Tukutane saa nane kamili Protea Hotel karibu na St. Peter ntakutana na Wanahabari. Karibuni sana!

chanzo:Mpekuziblog.

Comments