Kikosi kazi kusimamia uchimbaji mchanga Zanzibar.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mazingira, Mifugo na Uvuvi, Zanzibar , Dk Islam Seif  Salum amesema kuanza kwa uchimbaji mchanga viwani hapa  kutaondoa wizi wa mchanga maeneo mbalimbali.


Ruhusa hiyo imekuja ikiwa ni  takriban mwezi mmoja tangu kupigwa marufuku uchimbaji mchanga visiwani hapa.

Uchimbaji unafanyika katika maeneo ya Mkoa wa Kaskazini Unguja, ambako viongozi wa Serikali wameonekana kusimamia shughuli hiyo ili ifanyike kwa amani na utulivu.

Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini B, Issa Juma Ali amesema kikosi kazi cha usimamizi kitahakikisha kazi hiyo inafanyika kwa mpangilio.

Baadhi ya wamiliki wa magari ya mchanga, wamesema licha ya Serikali kufuta marufuku hiyo, utaratibu uliowekwa siyo mzuri.

Mmiliki wa gari, Juma Ahmada amesema utaratibu wa Serikali kusimamia uchimbaji ni mgumu hasa katika suala la kupanga bei.


chanzo:Mwananchi

Comments