Sambamba na kulaani mauaji hayo, Rais Museveni ametoa agizo hilo la
kufungwa CCTV katika maeneo muhimu ya nchi, hatua inayotazamiwa kutoa
mchango mkubwa katika kuimarisha usalama nchini humo.
Naibu Inspekta Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Uganda Felix Kaweesi
alipigwa risasi na kuuawa na watu wasiojulikana Ijumaa ya jana.
Duru za
kiusalama zinaarifu kuwa, Kaweesi ambaye pia ni Msemaji wa Polisi
aliuawa baada ya gari lake kumiminiwa risasi na watu wasiojulikana
alipokuwa anaondoka kwake nyumbani Kulambiro,
Kisaasi kaskazini,
mashariki mwa mji mkuu Kampala, ambapo aliuawa pamoja na walinzi wake
wawili walioandamana naye.
Habari zaidi zinasema kuwa, Naibu Inspekta Mkuu wa Polisi wa Uganda
alikuwa njiani kwenda kuwahutubia wanafunzi katika chuo kikuu cha Uganda
Christian University alipokumbana na mauti yake.
Vyombo vya usalama katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki vimeanzisha uchunguzi kubaini kiini na wahusika wa mauaji hayo.
Chanzo:parstoday.
Comments