Dominik
Stillhart, Mkurugenzi wa Operesheni za Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu
amesema kuwa, iwapo hatua za dharura hazitachukuliwa katika kipindi hicho,
mamilioni ya raia wa Somalia na Yemen watapoteza maisha kutokana na njaa.
Akiongea na
waandishi wa habari mjini Geneva, afisa huyo wa Msalaba Mwekundu amesema
shirika hilo linahitaji dola milioni 300 za Marekani kwa ajili ya msaada wa
chakula kwa watu wanaokabiliwa na baa la njaa lililosababishwa na ukame katika
nchi mbili hizo.
Ameongeza
kuwa, watu milioni 20 hususan wanawake na watoto wadogo wapo katika hatari ya
kufa njaa katika nchi hizo, pamoja na Sudan Kusini na Nigeria.
Kamati ya
Kimataifa ya Msalaba Mwekundu imesema kuwa, kufikia sasa, imepokea dola milioni
100 za Marekani pekee kati ya milioni 400 inazohitaji ili kushughulikia hali
hiyo ya kibinadamu katika nchi hizo tatu za Afrika na Yemen.
chanzo: parstoday.
Comments