Hayo yamedokezwa na Jawad Al Talibawi kamanda wa Wapiganaji wa vikosi vya kujitolea vya wananchi Iraq maarufu kama Al-Hashd Al-Shaabi ambaye ameongeza kuwa, wanajeshi wa Marekani wamemsaidia Abubakar Al Baghdadi kutoroka na kujificha katika eneo la Al-Qayrawan.
Amesema taarifa za kijasusi zinaonyesha kuwa kinara huyo wa ISIS yuko baina ya Al-Qayrawan na eneo la Al Hadhr yapata kilomita 80 kusini mwa Mosul.
Siku ya Jumatano, Wizara ya Ulinzi ya Marekani, Pentagon ilisema kuna uwezekano kuwa Al Baghdadi ameondoka Mosul na kujificha katika maeneo ya jangwani nje ya mji huo.
Siku chache zilizopita Al Baghdadi alitoa hotuba ya mwisho akikiri kushindwa kundi hilo nchini Iraq na akiwataka wafuasi wake kukimbilia maeneo ya milimani kwa usalama wao au kujiripua.
chanzo:parstoday.
Comments