
Ameyazungumza hayo jana kwenye ofisi za chama hicho zilizopo Vuga mjini Zanzibar,
Mazrui alisema katiba ya chama chao haimpi mwenyekiti uwezo wa kuwavua uongozi hivyo aliwataka wanachama wa Cuf kupuuza uamuzi huo.
Aidha alisema, Profesa Lipumba anafahamu kuwa hana uwezo wowote ndani ya chama hicho kisheria,hivi sasa licha ya kuwa bali lengo lake ni kuhakikisha anakihujumu Chama kwa kutumia mbinu mbalimbali kwa maslahi binafsi.
Alisema katika Katiba ya Cuf Ibara ya 9(i) na (f), inaeleza kuwa mwenyekiti ana uwezo wa kuteua nafasi mbalimbali kama wakurugenzi, manaibu wao na viongozi wengine, lakini haimpi uwezo wa kumvua uongozi kiongozi aliyemteua bila ya idhini kutoka kwa kamati ya utendaji ya chama na kuridhiwa na wajumbe wa Baraza Kuu.
Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano ya Umma wa Cuf, Salum Biman alisema anachokifanya Profesa Lipumba amekua anashangaza sana watu licha ya kuwa anafahamu si kiongozi ni mwanachama wa Cuf.
chanzo:zanzibar24.
Comments