Mahakama ya
Hakimu Mkazi Tanga itaanza kusikiliza utetezi wa Wakili Alfred Akaro baada ya
kumuona ana kesi ya kujibu kuhusu shauri la kughushi wasia wa marehemu Mohamed
Shosi lililofunguliwa na mjane huyo aitwaye.
Akaro alikuwa
wakili wa Saburia Shosi ambaye ni mtoto wa marehemu katika kesi ya madai ya
mirathi ya Mohamed Shosi iliyofunguliwa mahakamani hapo.
Katika shauri
hilo la jinai namba 10/2016, mjane huyo anamlalamikia wakili huyo na Aboubakar
Shaaban kwamba wameghushi wasia uliokuwa umeandikwa na Shosi kuhusu mirathi ya
mali zake.
Hakimu Mfawidhi
wa mahakama hiyo, Aziza Lutala ametoa uamuzi wa shauri hilo baada ya kupitia
malalamiko yaliyowasilishwa mahakamani na kusema ameona wakili hiyo ana kesi ya
kujibu.
chanzo:Mwananchi.
Comments