Ghala hilo lililo eneo la Balakliya liko umbali wa karibu kilomita 100 kutoka eneo la mapigano na waasi wanounga mkono Urusi.
Hutumika kuhifadhi maelfu ya tani ya risasi na makombora.
Makundi ya uokoaji yanaongoza shughuli kubwa ya kuwahamisha watu wanaoishi mji huo na vijiji vilivyo karibu.
Silaha kutoka ghala hilo hutumiwa na vikosi vilivyo eneo la mzozo katika maeno yaliyo karibu ya Luhanks na Donetsk.
Mamlaka
inachunguza njia tofauti milipuko hiyo ilisababishwa. waziri wa ulinzi
Stepan Poltorak alisema kuwa kuna uwezekano wa kifaa cha kulipuka
kuangushwa na ndege isiyokuwa na rubani.
Ndege isiyokuwa na rubani inaripotiwa kutumika kujaribu kuwasha moto ghala hilo mwezi Disemba mwana 2015.
chanzo:Bbc.
Comments