Maalim Seif: CUF haina mpango wa kufanya mazungumzo na Lipumba.

Katibu mkuu wa  CUF Maalim Seif Sharif Hamad amesema Chama cha wananchi CUF hakina mpango wa kufanya  mazungumzo na Mwenyekiti anaetambuliwa na Msajili wa vyama vya siasa nchini  Professa Ibrahim lipumba  kwani yeye ndie chanzo cha kutaka kukivuruga chama hicho.

Akizungumza na Waandishi wa habari amesema migogoro yote kwenye chama hicho imesababishwa na Lipumba akiwa na lengo la kukivuruga chama kwa makusudi na kudai kuwa ametumwa na vyama vya upinzani.
Hata hivyo amesema chama cha CUF kimefanyiwa hujuma mbalimbali ili kivunjike moyo katika majukumu yake ya kutaka kuchukua dola ili kuwapa wazanzibar haki zao na kuahidi kuwa mabadiliko yatakuja Zanzibar baada siku chache zijazo.
chanzo:Zanzibar24

Comments