Maalim Seif ampiga marufuku Lipumba Kukanyaga Mtendeni.

Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Hamad amempiga marufuku Prof. Lipumba kukanyaga Makao Makuu ya Chama hiko yaliyoko Mtendeni, Zanzibar.
Amedai kuwa amepata taarifa kuwa Lipumba anasema ana wafuasi wengi visiwani humo lakini yeye na wanachama wengine watayalinda Makao Makuu hayo muda wote na hatoweza kuingia.

Amesema jukumu la kulinda Makao Makuu hayo si la mtu mmoja bali la kila ambaye anajali maslahi ya chama.
chanzo:zanzibar24.

Comments