Msemaji wa
Wizara ya Afya ya Zambia amesema kuwa maafisa wa wizara hiyo wamewataka
wananchi kutilia maanani usafi na taratibu za kinga ili kuzuia maambukizi zaidi
ya ugonjwa wa kipindupindu.
Ameongeza
kuwa, watu walisiopungua 70 wameambukizwa ugonjwa huo na kwamba kuna uwezekano
ukaenea zaidi katika maeneo mengine.
Wakati huo
huo serikali ya Zambia imetangaza kwamba imefunga shule kadhaa na vituo vya
uvuvi katika mkoa Luapula ili kuzuia maambukizi ya kipindupindu.
Waziri wa
Afya wa Zambia, Chitalu Chilufya amesema kufungwa kwa shule hizo ni sehemu ya
hatua za kudhibiti mlipuko wa kipindupindu katika mkoa wa Luapula ambapo makumi
ya kesi za ugonjwa huo zimeripotiwa katika wiki nne za hivi karibuni.
Hali duni ya
usafi na mazingira machafu vinatajwa kuwa sababu ya mlipuko wa kipindupindu
katika maeneo yenye watu wengi nchini Zambia.
chanzo: parstoday.
Comments