Kauli na Maagizo ya Waziri wa mambo ya ndani dhidi ya askari aliemtolea bastola Nape.

Waziri wa mambo ya ndani Mhe. Mwigulu Nchemba ameonesha kusikitishwa kwake na kitendo cha askari kumtolea bastola aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye kwa kusema kitendo hicho si cha kiaskari, sio cha kitanzania na sio cha kimungu.

Aidha Waziri Nchemba amesema iwapo mtu huyo ameweza kutoa bastola mbele ya kamera, je ingekuwa kwenye uchochoro angefanya nini.


Wakati huohuo Mhe. Nchemba amemuagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP kumsaka mtu huyo aliemtolea bastola Mhe. Nape na akigundulika kuwa ni askari kweli basi hatua za Taasisi husika zichukue mkondo wake.

 Chanzo:zanzibar24.

Comments