Aidha, kamati hiyo imeagiza ripoti ya ukaguzi huo ipelekwe kwao kabla
ya kuanza kwa vikao vya Bajeti vya Bunge, Aprili 4, mwaka huu mjini
Dodoma.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Peter Serukamba alitoa agizo hilo jijini
Dar es Salaam baada ya kutembelea DIT ili kuona utekelezaji wa mradi wa
ujenzi huo akiambatana na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na
Mafunzo ya Ufundi, Stella Manyanya.
Alisema ipo haja ya serikali kufanya ukaguzi wa kina katika mradi huo
kutokana na kuchukua muda mrefu kuanzia mwaka 2008 hadi sasa bila
kukamilika licha ya kubainika kuwa fedha zilikuwa zimetolewa.
“Mradi huu ulianza kwa awamu ya kwanza mwaka 2008 ukitakiwa
kukamilika ndani ya mwaka mmoja, lakini baadae ukasimama, awamu ya pili
ukaanza mwaka 2012 ikipangwa kukamilika mwaka 2013 kutokana na kutopata
fedha kutoka serikali ulisimama na kuanza tena mwaka 2016,” alisema
Serukamba.
Alisema licha ya mradi huo kukumbwa na changamoto ya kucheleweshewa
fedha, lakini serikali ilipotoa fedha mwaka jana, hakukuwa na bodi
iliyotakiwa kuidhinisha zabuni za ujenzi pamoja na kujua kupanda kwa
gharama za ujenzi kutoka Sh bilioni 5 za awali na kufikia Sh bilioni 7
za sasa.
Aliongeza kuwa licha ya Mkuu wa DIT, Profesa Preksedis Ndomba kukiri
kuwa pamoja na changamoto mbalimbali za mradi huo, lakini chuo kina
fedha ambayo iko benki, lakini akashindwa kufafanua kama inaweza
kukamilisha ujenzi wa jengo hilo lenye urefu wa ghorofa 10.
Alisema lengo la mradi ni kuongeza udahili wa wanafunzi wapatao 984
na ofisi za walimu 46 na limekamilika kwa asilimia 80. Naibu Waziri
Manyanya aliahidi kufanyia kazi maagizo ya kamati ambayo imekuwa
ikifanya jitihada ili mradi huo ukamilike.
chanzo:Habarileo.
Comments