Jumuiya sita
za kimataifa zikiwemo za International Solidarity na Action Against Hunger
zimetangaza katika kikao kilichofanyika jana mjini Paris,
Ufaransa kwamba
mgogoro wa Yemen unaelekea kuwa moja kati ya migogoro mikubwa zaidi ya wanadamu
katika dunia ya sasa.
Taarifa
iliyotolewa na jumuiya hizo imesema jumuiya za misaada ya kibinadamu
zinakabiliwa na matatizo makubwa nchini Yemen kuliko eneo lolote jingine
duniani.
Hivi karibuni
pia taarifa ya Umoja wa Mataifa ilisema kuwa, njaa, vizingiti vya aina
mbalimbali na kuzuiwa operesheni za misaada ya kibinadamu kupelekwa kwa
waathirika, na mashambulizi yanayoendelea kufanywa na Saudi Arabia na washirika
wake dhidi ya watu wa Yemen vimeitumbukiza nchi hiyo katika mgogoro mkubwa.
Taarifa hiyo imesema kuwa watu milioni 26 ambao hata kabla ya kuanza vita
nchini Yemen walikuwa wakikabiliwa na umaskini, sasa wanasumbuliwa na hali
mbaya zaidi.
Taarifa ya
Umoja wa Mataifa inasema zaidi ya nusu ya hospitali na vituo vya afya nchini
Yemen vimeharibiwa kwa mashambulizi ya Saudi Arabia na kwamba raia wa kawaida
wanasumbuliwa na maradhi ya aina mbalimbali yakiwemo ya kipindupindu na
utapiamlo.
Saudi Arabia
inaizingira Yemen kutoka pande zote za anga, nchi kavu na baharini na inazuia
kuingizwa misaada ya kibinadamu nchini humo.
chanzo: parstoday.
Comments