Katika taarifa
iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu,
Rais Magufuli amesema wamezungumza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kumtakia
heri ya siku ya kuzaliwa Dk.
Kwa upande wake
Rais Dkt. Ali Mohamed Shein amesema anamshukuru Rais Dkt.Magufuli kwa kumtakia
heri katika siku yake muhimu ya kuzaliwa na hivyo wamekutana kubadilishana
mawazo katika kuhakikisha wanajenga nchi na kusonga mbele.
''Siku ya
kuzaliwa ni siku ya furaha lazima ikumbukwe lazima isherehekewe, mimi siku
yangu ya kuzaliwa sisherehekei sana lakini huwa nafurahi sana na leo
nimefurahi sana'' amesema Dkt. Shein.
Shein amesema
ametumia siku yake ya kuzaliwa kumtembelea Rais Dkt.Magufuli ili waweze
kubadulishana mawazo kwani wana kazi kubwa ya kujenga nchi.
chanzo:Mwananchi.
Comments