
Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kamanda wa polisi mkoa wa Mjini
Magharibi Kamishna Msaidizi Mwandamizi Hassan Nassir Ali amesema jeshi
la polisi limejipanga kumaliza uingizaji, usambazaji na matumizi ya dawa
za kulevya katika Mkoa wa mjini magharibi kabla kumalizika mwaka 2017.
Kamanda Nassir amesema jeshi hilo limejipanga kikamilifu kuhakikisha linamaliza tatizo hilo haraka iwezekanavyo na kuwaomba wananchi wa mkoa huo kuunga mkono juhudi za jeshi la polisi katika kufikia malengo waliyojiwekea.




chanzo:zanzibar24.
Comments