Freeman Mbowe: Paul Makonda hana sifa za kuuongoza mkoa wa Dar es Salaam.

FreemanMbunge wa Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe amesema kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda hana tena sifa  za kuuongoza mkoa huo kutokana na mwenendo wake ambao haukubaliki.

Mbowe ameyasema kufuatia tuhuma nyingi zilizoibuka hivi karibuni kuhusu kiongozi huyo. 


Miongoni mwa tuhuma hizo ni kuhusu uhalali wa vyeti vya Makonda, uongozi wake usiofuata sheria za utawala bora, matumizi mabaya ya mali za serikali, utajiri usio na majibu  pamoja na kuingilia uhuru wa vyombo vya habari.

Baadhi ya viongozi na wadau wengine pia wamelizungumzia suala hili kuwa siyo la kufumbiwa macho huku wakimtaka Rais Dkt John Pombe Magufuli kumchukulia hatua kiongozi huyo. 

Miongoni wa viongozi waliotoa maoni yao ni pamoja na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Tundu Lissu ambapo amemtaka Rais Dkt Magufuli kutengua uteuzi wa Makonda.

Licha ya tuhuma zote hizo kutolewa na vyombo vya habari pamoja kwenye mitandao ya kijamii, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda hajasema lolote kuhusiana hayo yanayozungumzwa, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma haijazungumza wala Baraza la Mitihani la Tanzania.

chanzo: zanzibar24.

Comments