Katika mahojiano kwa njia ya Televisheni amesisitiza kuwa kampeni
zake zitaendelea ingawa amekuwa akipata upinzani kutoka kwa baadhi ya
wanachama wa Republican.
Viongozi wa chama watakutana siku ya
Jumatatu kuamua cha kufanya huku baadhi wakitaka aliyekuwa waziri mkuu
wa Ufaransa Alan Juppe' kuchukua nafasi ya Fillon.
Bwana Juppe amesema atatoa tamko siku ya Jumatatu.
Baadhi
ya watu wanaomuunga mkono bwana Fillon wametishia kura zao kuzipeleka
kwa mgombea wa chama cha National Front iwapo watamshinikiza kuondoka.
Chanzo:bbc.
Comments