Diwani anusa mchezo mchafu kutoapishwa kwake.

HABARIDiwani wa Iganjo (Chadema), David Mwangonela amesema uamuzi wa Serikali jijini hapa kuliengua jina lake kwenye kikao cha Baraza la Madiwani ili asiapishwe umefanywa kwa msukumo wa kisiasa.



Akizungumza nje ya ukumbi wa mikutano wa Benjamin Mkapa kilipofanyika kikao hicho, Mwangonela alisema tangu ashinde rufaa Desemba 17 mwaka jana hajawahi kupewa au kuambiwa kwamba amekatiwa rufaa na kwamba, kuibuka kwa hoja hiyo katika kikao hicho ni mwendelezo wa fitina za kisiasa.



Diwani huyo alihukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela mwaka 2015 baada ya kutiwa hatiani na Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya, Novemba 17, 2015 kwa kosa la kuvunja ghala na kuiba magunia 171 ya ngano mali ya Chuo cha Utafiti na Kilimo Uyole.



Hata hivyo, alikata rufaa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya na alishinda Desemba mwaka jana baada ya Jaji Mfawidhi wa mahakama hiyo, Noel Chocha kuamuru arejeshwe udiwani wake.


Mwanasheria wa Jiji la Mbeya, Davis Mbembela alisema diwani Mwangonela asingeweza kuapishwa kwa kuwa baada ya kushinda, Jamhuri ilikata rufaa hivyo bado anakabiliwa na kesi.


chanzo;Mwananchi.

Comments