Rais el-Sisi ameyasema hayo mjini Cairo, katika mkutano wa pamoja wa waandishi wa habari akiwa na Kansela wa Ujerumani Bi, Angela Merkel na kuongeza kuwa, nchi za eneo la Mashariki ya Kati zinazounga mkono magaidi, zinatakiwa kukomesha mwenendo huo.
Akisisitizia udharura wa kulindwa umoja wa ardhi ya Syria na kuharakishwa ukarabati wa nchi hiyo, amezitaka nchi waungaji mkono wa ugaidi kuacha hatua zao hizo.
Kwa upande wake, Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel amesema kuwa, kamwe mgogoro wa Syria hauwezi kutatuliwa kwa njia ya kijeshi na badala yake unatakiwa kutatuliwa kwa njia za kisiasa chini ya usimamizi wa Umoja wa Mataifa.
Safari ya Bi, Merkel nchini Misri pia ilikuwa na lengo la kuishawishi Cairo kuungana na mpango wa kupambana na wahajiri haramu kuelekea barani Ulaya. Hii ni katika hali ambayo kabla ya Kansela wa Ujerumani kufanya safari hiyo nchini Misri, Shirika la Msamaha Duniani (Amnesty International) lilikuwa limemtaka Bi, Merkel kuzungumza na Rais el-Sisi kuhusiana na faili la ukandamizaji wa haki za binaadamu nchini Misri.
chanzo:parstoday.
Comments