Zaidi ya Shillingi Millioni 200 na 15 wamekebidhiwa wananchi wa Jozani kwa maendeleo ya vijiji vya hifadhi ya jozani .
Akisoma risala ya wanakijiji wa Jozani, wakati wa mgao wa Fedha wa hifadhi ya misitu Mussa Saleh Mihambo amesema takribani miaka 16
wanakijiji wanamefaika kupitia msitu huo katika hivi sasa kumejitokeza watu kuuhujumu msitu kwa kufanya vitendo vya uwindaji holela wa wanyama na ukataji wa miti,Uvamizi wa maeneo ya misitu kwa kisingizio cha kuimarisha kilimo,Ujenzi holela wa nyumba za makaazi unaosababisha uharifu wa misitu na yote hayo yamesababishwa na ulinzi duni wa msitu wa hifadhi ya taifa jozani.
Nae Mkuu wa wilaya ya Kati Mashavu Sukwa amesema nikweli msitu unaharibiwa na kukatwa kwa kasi kubwa katika maeneo hayo na kusababisha uharibifu wa mazingira na kupelekea kushuka kwa pato la taifa hivyo amesema ili kunusuru hali hiyo nivyema katika maeneo hayo ya misitu kufungwe nyuki ili kunusuru hali hiyo kwalengo la kuuhigfadhi.
Kwaupande wake Waziri wa kilimo Mali asili mifugo na uvuvi Hamad Rashid Mohamed amesema kutokana na matatizo hayo Serikali ya Mapinduzi zanzibar itachukua hatua za kisheria kwa kuwafikisha watenda hujuma katika vyombo vya sheria ili kudhibiti rasilimali hizo ambazo zinaingiza pato la taifa kupitia Fedha za kigeni.
Aidha amesema chanzo cha matatizo hayo yote ni wanajamii kutokuwa na utayari kushirikiana na serikali katika hatua mbalimbali za maendeleo kwa kuwafichua wahalifu na badala yake huendekeza Muhali na kupelekea athari kubwa katika hifadhi.
Zaidi ya Shillingi Million 200 na 15 wamekebidhiwa wananchi wa Jozani kwa maendeleo ya vijiji vya hifadhi ya jozani kwa lengo la kubuni miaradi ya maendeleo.
chanzo:ZANZIBAR24
Comments