Zaidi ya asilimia 80 ya wanawake wajasiriamali hufanyiwa ukatili.

Imeelezwa kuwa zaidi ya asilimia 80 ya wafanyabiashara wa kike katika masoko hunyanyaswa na kufanyiwa ukatili husasani  kutolewa lugha chafu hali inayowarudisha nyuma kimaendeleo.



Mratibu wa Shirika la kuwatetea wanawake, la Equality for Growth (EfG), Ikupa Mwakisu amesema wanawake hao wanaofanya shughuli zao masokoni hufanyiwa ukatili.



“Utafiti uliofanywa na shirika hili na kuhusisha masoko ya Soko Kuu, Mlango mmoja na Kirumba ya jijini Mwanza, mwaka 2014/15 ulionyesha asilimia kubwa wanawake hufanyiwa vitendo vya kikatili na kuwasababishia kufanya kazi zao katika mazingira magumu,” amesema Mwakisu.
chanzo:Mwananchi.

Comments