Wakuu wa Mikoa na Wilaya watakiwa kutumia sheria katika udhibiti uchimbwaji mchanga.

Waziri wa kilimo Maliasili Mifungo na Uvuvi Zanzibar  Hamadi Rashid Mohammed amesema kutokana na hali mbaya iliyopo ya uchimbaji mchanga  hivi sasa  ipo haja kwa viongzi wote  kutumia sheria  katika kudhibiti  watu wanaochimba  rasilimali hiyo kinyume na sheria.

Akizungumza katika kikao maalumu na Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya pamoja na Makamanda wa Jeshi la polisi amesema  kuna baadhi ya viongozi  hawasimamii vyema  sheria katika kufanya kazi na badala yake  kufanya kazi kwa maslahi yao binafsi.

Hivyo amewataka wakuu hao , jeshi la polisi pamoja na Masheha   kuzingatia  utaratibu uliowekwa na serikali  katika utoaji vibali  ili  serikali iweze kunufaika na mapato  pia  kuzidisha ulinzi  katika maeneo
yanayochimbwa mchanga  na yale  maeneo   yasio rasmi kuchimbwa.

Kwa upande wao Wakuu wa Mikoa Mitatu ya Unguja Ayoub Mohamed Mahmoud, Dk. Idrisa Muslih Hija na Vuai Mwinyi wamesema kutokana na janga hilo  hawatamfumbia mtu macho katika  kudhibiti uchumbwaji mchanga hasa wale wanaochimba kinyume na sheria  bila ya kibali maalum kutoka serikalini.

Kikao hicho kilichowakutanisha Waziri wa kilimo, MaDC wa mikoa yote unguja, MaRC pamoja na Jeshi la polisi kinalengo la kutafuta njia za kudhibiti rasilimali hiyo kutotoweka hapa zanzibar.

CHANZO:Zanzibar24 .

Comments