
Akiuliza swali katika kikao cha baraza la wawakilishi alipotaka kujua ni mashahidi wangapi ambao wanadai posho zao na ni lini serikali itawalipa posho hilo
amesema mashahidi ni sehemu muhimu katika kesi lakini kumekua na malalamiko makubwa kwa mashahidi hao kudai posho lao kwa muda mrefu
Akijibu swali hilo naibu waziri wa nchi ofisi ya rais katiba sheria utumishi wa umma na utawala bora Hamis Juma Mwalimu amesema serekali inatambua umuhimu wa mashahidi katika uendeshaji wa kesi mahakamani hivyo inaendelea kuwalipa fedha mashahidi hao kwa awamu kadri ya fedha itakavyoruhusu.
Jumla ya shilling million nne na laki tano zimetengwa kwa ajili ya kuwalipa mashahidi kupitia idara ya mahakama ambapo jumla ya mashahidi 53 wanadai posho zao kwa kipindi cha miezi mitatu.
chanzo:Zanzibar24.
Comments